8. Ingawa mtihani ni muhimu mno katika mfumo wowote ule wa elimu, ni muhimu kutaja kwamba, kwa sababu ya kusisitiza sana umuhimu wa mitihani visa vya udanganyifu katika mitihani yenyewe vimeshuhudiwa. Baadhi ya wanafunzi huhiari kunakil majibu kutoka vitabuni ili kuipita mitihani yao na kujiunga na shule auvyuo mbalimbali. Wazazi wengine huwalipa watu fulani kufanyia watoto wao mitihani. Hivi ni vitendo visivyokubalka. Kila mwaka matokeo ya mitihani yanpotangazwa, hatukosi kusikia kuwa shule fulani haikupata matokeo kwa sababu ya visa vya udanganyifu. Hali inapokuwa hivyo, wanafunzi husika hulazimika kurudia mitihani baadaye. Huu ni ubadhirifu wa wakati na mali. Hali kadhalika, mitihani japo hupima uwezo wa mwanafunzi katika masomo fulani hauwezi kutumiwa kama kigezo tosha cha kututhamini umilisi wa mwanafunzi. Wapo baadhi ya wanafunzi ambao ni hodari masomoni lakini huenda wasifanye vyema katika mitihani. Jambo hili huweza kusababishwa na hali ya afya ya mwanafunzi wakati mtihani, faadha au uchechefu wa karo. Baadhi ya watu ambao hawakufua dafu katika mitihani huenda wakawa watendakazi wema.
Mitihani huhitaji matayarisho ya dhati. Mwalimu pia ana jukumu pia la kumsaidia mwanafunzi katika matayarisho kwa kuhakikisha kuwa amemwelekeza kuhusu jinsi ya kukabiliana na aina mbalimbali za maswali na jinsi ya kuutumia muda wake. Aidha, mwalimu anahitajika kumshuri ni somo gani linalohitaji kushughulikiwa kwa makini zaidi. Ni muhimu pia mwalimu amshauri mwanafunzi jinsi ya kudurusu na kujihusisha katika michezo mbalimbali ili kupumzisha ubongo. Juu ya yote hayo, ni muhimu mwanafunzi kujua kwamba anahitaji lishe bora ili kupata nguvu za kuyatalii masomo na kuikabili mitihani yake.
Binadamu hana budi kufanya mitihani mbalimbali aushini mwake. Hata hivyo, haifai kuichukua mitihani kama kibali cha kuwabagua watoto. Baadhi ya wana jamii huwadharau watoto wasiofanya vyema katika masomo yanayostahiwa na jamii hiyo. Watu kama hawa huwatia watoto kiwewe na kutojiamini. Wazazi wengine hata huwalazimisha watoto wao kusomea taaluma ambazo wao wazazi wanazipendelea. Jambo hili huwafanya wana hawa kusagika kufanya masomo wasiyoyamudu vyema. Wanaofanya vyema hushehnezwa sifa belele mbele ya ndugu zao pasi kujali hisia za ndugu hao . Jambo hili huzua uhasama miongoni mwa ndugu-uhasama ambao usipoangamizwa huleta hasara katika familia. Hatuna budi kuitumia mitihani kumkuza binadamu bali si kumviza.
Ni kweli kusema kuwa?